Alhamisi, 25 Septemba 2014

TAASISI YA VOTER'S VOICE ORGANIZATION (SAUTI YA MPIGA KURA) YAZINDULIWA RASMI DAR ES SALAAM LEO

TAASISI YA VOTER'S VOICE ORGANIZATION (SAUTI YA MPIGA KURA) YAZINDULIWA RASMI DAR ES SALAAM LEO

 Steven Mwasomola Mkurugenzi Mkuu wa Voter's Voice Organization.
Mwenyekiti wa Voter's Voice Organization
  Alfred Luvanda. (Imeandaliwa na mtandao wa 
habari za jamii.com-simu namba 0712-727062)
 Ofisa Mawasiliano wa Voter's Voice Organization, 
Andrew Mwakalebela.
 Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Sauti ya Mpiga Kura ((Voters Voice Organization), Steven Mwasomola (kushoto), akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari Dar es Salaam leo, wakati wa hafla ya kuzindua taasisi hiyo. Kulia ni Mwenyekiti wa Jukwaa la Katiba Tanzania (Jukata), Deus Kibamba. 
 Mwenyekiti wa Voter's Voice Organization,  Alfred Luvanda (katikati), akizungumza katika hafla hiyo ya uzinduzi wa taasisi hiyo. Kulia ni Katibu wa Voter's Voice Organization, Ikupa Njela na Mjumbe kutoka Jukwaa la Katiba Tanzania (Jukata), Hebron Mwakagenda.
 Mwenyekiti wa Jukwaa la Katiba Tanzania (Jukata), Deus Kibamba (kulia), akizungumza katika uzinduzi huo. Kushoto ni Katibu Mtendaji wa Taasisi ya TAYOAF, Gasper Mahekuka na Mkurugenzi Mkuu wa Voter's Voice Organization, Steven Mwasomola.
 Katibu Mtendaji wa Taasisi ya TAYOAF, Gasper Mahekuka akizungumza katika uzinduzi huo.
 Maofisa wa Voter's Voice Organization wakiwa 
kwenye uzinduzi huo.
 Maofisa wa Voter's Voice Organization wakiwa 
kwenye uzinduzi huo.

Dotto Mwaibale

VIJANA nchini wametakiwa kujitokeza kuhamasisha jamii katika utoaji wa elimu ya uraia na upigaji kura badala ya kuwaachia wazee wapige kura.

Mwito huo umetolewa na Mwenyekiti wa Taasisi ya Sauti ya Mpiga Kura (Voters Voice Organization), Alfred Luvanda wakati akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam leo, kwenye hafla ya uzinduzi wa taasisi hiyo.

"Ni vema vijana wakajua elimu ya uraia na upigaji kura ili kutoa fursa kwa wananxchi wengi kupiga kura katika chaguzi mbalimbali badala ya kuwaachia wazee"alisema Luvanda.

Alisema watu wengi wanashindwa kujitokeza kupiga kura kwa sababu hawana elimu ya uraia na upigaji kura matokea yake wanaochaguliwa kuongoza wanakuwa na idadi ndogo ya watu waliowachagua.

Akizungumza kuhusu taasisi hiyo, Meneja Mawasiliano wa Taasisi hiyo Andrew Mwakalebela alisema haifungamani na chama chochote cha siasa, kidini na mtu yeyote anayeshiriki siasa.

Alisema taasisi hiyo imejikita katika mambo makuu matatu ambayo ni ya kijamii, Kisiasa na kiuchumi na kutoa elimu ya uraia na kupiga kura.

Mwakalebela alisema kazi nyingine ya taasisi hiyo kuimarisha demokrasia ya ukweli kwa kuwaasa wananchi kuepuka kuuza kura na kuwa chombo cha kuwasemea wananchi pamoja na kuitangaza amani ya nchi na kuilinda wakati wote.

Jumamosi, 8 Februari 2014

RAIS ATANGAZA MAJINA YA WAJUMBE WA BUNGE LA KATIBA MPYA


UTANGULIZI

1. Uteuzi wa Wajumbe wa Bunge la Katiba Unatawaliwa na Sheria ya Mabadiliko ya Katiba, Sura, 83 (The Constitutional Review Act, Cap 83). Sheria hii inaweka mamlaka ya uteuzi, masharti, taratibu, vigezo na mambo mengine yote yanayopaswa kuzingatiwa katika uteuzi wa Wajumbe wa Bunge la Katiba. Kwa mujibu wa Kifungu cha 22 (2A) na (2B) vigezo hivi vinajumuisha umri, jinsia, uzoefu, sifa na mahali anapotoka mjumbe husika.



2. Sheria hii inatamka aina tatu za Wajumbe wa Bunge la Katiba kama ifuatavyo:


(i) Wabunge wote wa Bunge la Jamhuri ya Muungano;

(ii) Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi la Zanzibar; na

(iii) Wajumbe 201 kwa mujibu wa Kifungu Na. 22(1c) cha Sheria ya Mabadiliko ya Katiba ambayo inaonyesha makundi mbalimbali 10 yanayohusika.



3. Makundi hayo ni kama ifuatavyo:-



(i) Taasisi zisizokuwa za Kiserikali (20)

(ii) Taasisi za Kidini (20)

(iii) Vyama vyote vya Siasa vyenye Usajili wa Kudumu (42);

(iv) Taasisi za Elimu (20);

(v) Watu wenye Ulemavu (20);

(vi) Vyama vya Wafanyakazi (19);

(vii) Vyama vinavyowakilisha Wafugaji (10);

(viii) Vyama vinavyowakilisha wavuvi (10);

(ix) Vyama vya Wakulima (20); na

(x) Vikundi vya Watu wenye Malengo yanayofanana (20).



4. Mchakato wa uteuzi ulianza kwa kutoa Tangazo la Mwaliko katika Gazeti la Serikali, Tangazo la Serikali Na 443 la tarehe 13 Desemba, 2013. Tangazo hilo lilitolewa kwa lugha ya Kiswahili na Kiingereza ili kuyaalika makundi yaliyotajwa kisheria kuwasilisha mapendekezo ya majina kwa ajili ya uteuzi katika Bunge laMaalum la Katiba. Aidha, Tangazo hilo la mwaliko lilitangazwa pia katika magazeti mbalimbali yanayosomwa hapa nchini. Pamoja na mambo mengine Tangazo la Mwaliko lilitamka ukomo wa muda wa Taasisi na Makundi kuwasilisha mapendekezo ya majina ya wajumbe kuwa ni tarehe 02/01/2014.

 

5. Mapendekezo hayo yalitakiwa kuwasilishwa kwa Katibu Mkuu Kiongozi wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa upande wa Tanzania Bara na kwa upande wa Zanzibar, mapendekezo yalitakiwa kuwasilishwa kwa Katibu Mkuu Kiongozi wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar.



6. Kufuatia mwaliko huo, taasisi 554 kutoka Tanzania Bara na 178 kutoka Zanzibar ziliwasilisha mapendekezo yao. Mapendekezo hayo yalijumuisha majina 2,762 kwa upande wa Tanzania Bara na kwa upande wa Zanzibar mapendekezo hayo yalihusisha watu 874. Hivyo basi, taasisi na makundi mbalimbali yalipendekeza jumla ya majina 3,636. Lakini, na kinyume na Sheria, watu 118 walijipendekeza wenyewe na kufanya idadi ya majina yaliyopendekezwa kuwa 3,754.



7. Mchanganuo wa idadi ya watu walipendekezwa katika makundi mbalimbali ni kama ifuatavyo:

***Orodha  ni  ndefu  sana. << BOFYA  HAPA  KUONA  MAJINA  HAYO >>


Bofya  hapo  juu

Jumanne, 31 Desemba 2013

TASWIRA ZA HAFLA YA KUKABIDHI RASIMU YA PILI YA KATIBA VIWANJA VYA KARIMJEE JIJINI DAR ES SALAAM


 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akilakiwa na Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba Mhe. Joseph S. Warioba mara baaada ya kuwasili katika viwanja vya Karimjee Hall kupokea Rasimu ya Pili ya Katiba. Kulia ni Mhe. Assaa Rashid, Katibu wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, 
 Rais Kikwete akisalimiana na Mhe Assaa Rashid, Katibu wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, 
 Rais Kikwete akisalimiana na Jaji Mkuu wa Zanzibar Mhe Omar Othman Makungu huku Jaji Mkuu wa Tanzania Bara Mhe Mohamed Chande Othman, Spika wa Bunge la Muungano Mhe Anne Makinda na Spika wa Zanzibar Mhe Pandu Ameir Kificho wakisubiri zamu zao
 Rais Kikwete akimuamkia  na Rais Mstaafu Alhaj Ali Hassan Mwinyi
 Rais Kikwete akimuamkia Waziri Mkuu Mstaafu Mhe Cleopa David Msuya
 Meza kuu
 Sehemu ya wajumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba
 Jukwaa kuu la pili
 Sehemu ya wajumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba
 Waziri Mkuu Mstaafu Dkt Salim Ahmed Salim akiwa na wajumbe wenzie wa Tume na maofisa wa serikali
 Dkt Asha Rose Migiro, Mama Amne Salim na Mama Warioba
 Sehemu ya wananchi walioshuhudia tukio hilo la kihistoria
 Wananchi wakiwa katika hafla hiyo
 Wananchi wakifuatilia hafla hiyo
 Watangazaji wa TBC wakiwa kazini kurusha live tukio hilo
 Baadhi ya wazee mashuhuri katika hafla hiyo. 
 Wadau mbalimbali
 Wadau katika hafla hiyo
 Sehemu ya viongozi wa vyama vya siasa
 Wadau wa habari 
 Wanasheria nguli, Mzee Mark Bomani na Profesa Issa Shivji wakiwa miongoni mwa wadau
 Balozi wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo Mhe Alfani Mpango akijumuika na wadau
 Baadhi ya viongozi wa vyama vya siasa na mabalozi
 Wadau na maafisa wa serikali
 Maafisa wa ofisi wa Msajili wa vyama na wadau
 Wadau wakifuatilia kwa makini kinachoendelea
 Wadau na maafisa mbalimbali
 Makatibu wakuu
 Waheshimiwa Mawaziri wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na Tanzania bara
 Waheshimiwa Mawaziri wa Tanzania Bara na Zanzibar
 Mawaziri, wabunge na maafisa wa serikali
 Sehemu ya mawaziri wa Tanzania bara na wa Zanzibar
 Msajili wa vyama vya siasa Jaji Francis Mutungi (wa tatu toka kushoto) akiwa ameketi na wabunge na viongozi wa vyama mbalimbali 
 Sehemu ya waliohudhuria hafla hiyo
 Meza kuu ikimsikilia Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba Mhe. Joseph S. Warioba 
 Rais Kikwete akimkabidhi Sir George Kahama nakala ya Rasimu ya Pili ya Katiba
 Rais Kikwete akiwakabidhi Mzee Hassan Nassoro Moyo na Jenerali Sarakikya nakala ya Rasimu ya Pili ya Katiba
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt Ali Mohamed Shein akisoma hotuba yake
 Rais Kikwete akihutubia
 Wabunge na wadau wengine wakifurahia hotuba ya Rais Kikwete
 Rais Kikwete, Rais wa Zanzibar Dkt Ali Mohamed Shein na Makamu wa Rais Dkt Mohamed Ghalib Bilali wakiwapongeza wajumbe wa Tume kwa kazi nzuri
 Picha ya pamoja ya viongozi wakuu na wajumbe wa Tume
 Picha ya pamoja ya viongozi wakuu, wajumbe wa tume 
 Viongozi wakuu, viongozi wa vyama vya siasa na wajumbe wa Tume
 Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue akisalimiana na Mhe Tundu Lissu
 Wajumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba 
 Rais Kikwete akiongea na Mwenyekiti wa CUF Profesa Ibrahim Lipumba na Mwenyekiti wa NCCR Mageuzi na Mbunge wa Kuteuliwa Mhe James Mbatia
Nikiripoti kutoka hapa katika viwanja vya Karimjee ni mimi....nanihii  wa Mlimani TV