Jumapili, 29 Desemba 2013

WAZIRI MKUU MSTAAFU SUMAYE APINGA RUSHWA KWA NGUVU KWENYE UCHAGUZI.

Rushwa kwenye chaguzi, ufisadi vyamchukiza Sumaye



‘“Ningefarijika sana kama tunaojiandaa kugombea nafasi mbalimbali hasa nafasi ya urais tungekemea rushwa na ufisadi hadharani.” Frederick Sumaye 
Na Daniel Mjema,Mwananchi

Posted  Jumapili,Decemba29  2013  saa 15:34 PM
Kwa ufupi
  • Sumaye alitoa kauli hiyo jana katika harambee ya kuchangia ujenzi wa ukumbi wa Parokia ya Mawela ya Kanisa Katoliki Jimbo la Moshi iliyohudhuriwa pia na Mbunge wa Moshi Vijijini, Dk Cyril Chami.
SHARE THIS STORY

1
Moshi. Waziri Mkuu Mstaafu, Frederick Sumaye amesema angefarijika kama wanasiasa wanaojiandaa kugombea Urais mwaka 2015, wangekemea vitendo vya rushwa na ufisadi hadharani.
“Zamani uongozi ulikuwa hautafutwi kwa udi na uvumba wala kwa rushwa, bali anayefaa kuwa kiongozi hutafutwa na jamii husika kutokana na ubora wake na siyo vishawishi vyake,” alisema Sumaye.
Sumaye alitoa kauli hiyo jana katika harambee ya kuchangia ujenzi wa ukumbi wa Parokia ya Mawela ya Kanisa Katoliki Jimbo la Moshi iliyohudhuriwa pia na Mbunge wa Moshi Vijijini, Dk Cyril Chami.
“Ni ukweli uliowazi kuwa, leo chaguzi zetu zimegubikwa na rushwa na vishawishi vingi na siyo ubora, uhodari wala tabia ya anayetaka nafsi hiyo ya uongozi,” alisema Sumaye na kuongeza kusema:
“Hivi sasa rushwa na matumizi makubwa ya fedha za kuwanunua wapiga kura vinataka kuwa utaratibu halali wa kuwapata viongozi wetu kuanzia ngazi za vijiji na mitaa hadi ngazi ya urais.”
Sumaye alisema Tanzania hivi sasa inaingia katika nyakati za uchaguzi hivyo, inahitaji viongozi watakaowaletea Watanzania maendeleo ya kweli na kuondokana na umasikini na udhalimu.
“Lakini kama tutakiuka taratibu sahihi za kuwapata viongozi na badala yake wapiga kura tukanunuliwa kwa kupewa rushwa, basi tujue tutawapata viongozi wala rushwa,” alisema Sumaye.
“Fadhila zimeanza kuwa nyingi, wapiga kura tayari wameanza kupigwa mnada na kupangiwa bei kulingana na uhodari au umuhimu wa nafasi aliyonayo mhusika,” alisisitiza Sumaye.
Sumaye alisema Jamii inapaswa kuyapiga vita mambo hayo kwa nguvu zote na kusema: “Vita hii ni kali na tusipoangalia sauti ya wanaopigana inaweza ikafifishwa na kelele za wanaonufaika na rushwa hizi za nyakati za chaguzi. Inaelekea fedha zinazotumika ni nyingi sana”.
“Ukikemea tu rushwa basi utapachikwa sababu nyingi zisizohusika ikiwemo ya kugombea urais mwaka 2015…nasema katika hili, suala la kugombea au kutogombea urais mwaka 2015 siyo sababu,” alisema.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni